IQNA

Misikiti Algeria yaanza kutayarishwa kwa ajili ya Mwezi wa Ramadhani

16:58 - February 06, 2021
Habari ID: 3473627
TEHRAN (IQNA) – Wizara ya Wakfu ya na Masuala ya Kidini Algeria imesema misikiti nchini humo ambayo ilifungwa kutokana na janga la COVID-19 sasa imeanza kutayarishwa kwa ajili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Kwa mujibu wa taarifa misikiti 3500 kati ya misikiti yote 18,000 Algeria ilifungwa kutokana na janga la corona na bado hakuna sala za jamaa katika misikiti hiyo.

Wizara ya Wakfu ya na Masuala ya Kidini Algeria inasema kufuatia kupungua maambukizi ya corona nchini humo baada ya kutekelezwa sheria za kutotoka nje, misikiti sasa itaanza kutafunguliwa hatua kwa hatua kuelekea katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Maimamu wa misikiti nchini Algeria kwa mara kadhaa sasa wametoa mwito kwa serikali kuruhusu misikiti ifunguliwe tena kufuatia kupungua maambukizi na pia baada ya kuanza zoezi la chanjo ya corona nchini humo.

3952010

captcha