Kwa mujibu wa taarifa vitabu hivyo vya Kiislamu vinasambazwa na jumuiya hiyo kwa lengo la kukabiliana na kile ambacho kinatajwa kuwa kukabiliana na nisimamo mikali na ya kigaidi nchini Comoro. Misaada hiyo ya itasambazwa miongoni mwa Makadhi, wanafunzi na maafisa wa serikali ya Comoro.
Sherehe ya kupokea vitabu hivyo vya Kiislamu na Misahafu imefanyika katika Kitivo cha Imam Shafii cha Chuo Kikuu cha Comoro.
Miongoni mwa walioshiriki katika sherehe hiyo ni Waziri wa Masuala ya Kiislamu Comoro Muhammad Hussein Jamalulayl na Sheikh Abdulkarim Mohammad Shakir mwenyekiti wa Jumuiya ya Kiislamu Comoro.